• HABARI MPYA

    Monday, February 10, 2014

    KIKOSI CHA TWIGA STARS KUAGWA FEB 12

    Na Boniface Wambura, Dar es Salaam 
    TIMU ya Twiga Stars itaagwa rasmi Jumatano (Februari 12 mwaka huu) tayari kwa safari ya Lusaka, Zambia kwa ajili ya mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya michuano ya Afrika kwa Wanawake (AWC) ambayo fainali zake zitafanyika Oktoba mwaka huu nchini Namibia. Msafara wa timu hiyo itakayoondoka kwa ndege ya Fastjet utaongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Ahmed Idd Mgoyi.

    Hafla ya kuwaaga wachezaji wa timu hiyo itafanyika saa 5 asubuhi kwenye ofisi za TFF. Timu hiyo itaondoka Februari 13 mwaka huu alfajiri tayari kwa mechi hiyo itakayochezeshwa na waamuzi kutoka Rwanda.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KIKOSI CHA TWIGA STARS KUAGWA FEB 12 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top