• HABARI MPYA

    Sunday, February 09, 2014

    AZAM FC WAWAFANYIA UUNGWANA YANGA, AL AHLY WALIKWENDA KUWAOMBA KUWEKA KAMBI CHAMAZI, WAKAWATOLEA NJE LEO MCHANA KWEUPE

    Na Mahmoud Zubeiry, Dar es Salaam
    AZAM FC imefanya kitu kimoja cha kiungwana sana kwa Yanga SC, baada ya kuwanyima Uwanja wa mazoezi klabu bingwa Afrika, Al Ahly ya Misiri.
    Kocha Msaidizi wa Ahly, ....akiiwa ameambatana na Maofisa wawili wa klabu hiyo walifika leo asubuhi makao makuu ya Azam, Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam kukagua hosteli ya klabu hiyo, Uwanja wa nyasi bandia na za kawaida na gym.
    Maofisa wa Al Ahly walikuwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jana kuiangalia Yanga SC ikimenyana na Komorozine.

    Baada ya hapo wakavutiwa na mandhari ya Azam Complex, hivyo kwenda kuomba kwa uongozi wa klabu hiyo watakapokuja kucheza na Yanga SC Machi mwaka huu waweke kambi kwa malipo mazuri.
    Hata hivyo, uongozi wa Azam ukawaambia hauwezi kufanya hivyo kwa sababu wapinzani wao,Yanga ni timu ya Tanzania hivyo hawawezi kuwasaidia wao (Ahly) maandalizi dhidi ya timu ya Watanzania wenzao.
    Baada ya kukwama Azam Complex, Maofisa hao wa Ahly wameeekeza nguvu zao Gymkhana na Shule ya Kimataifa ya (IST).
    Ahly inaweza kukutana na Yanga katika Raundi ya Kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika iwapo mabingwa hao wa Tanzania wataitoa Komorozine ya Comoro katika Raundi ya Awali.
    Yanga jana ilianza vyema katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Awali dhidi Komorozine kwa ushindi wa 7-0 na sasa wanahitaji hata sare ugenini au kufungwa si zaidi ya mabao 6-0 kusonga mbele, ambako watakitana na Ahly.  

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC WAWAFANYIA UUNGWANA YANGA, AL AHLY WALIKWENDA KUWAOMBA KUWEKA KAMBI CHAMAZI, WAKAWATOLEA NJE LEO MCHANA KWEUPE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top