• HABARI MPYA

    Tuesday, October 22, 2019

    VAN DIJK KUPAMBANA NA MESSI NA RONALDO KUWANIA BALLON D'OR

    NYOTA Cristiano Ronaldo, Lionel Messi, Mohamed Salah, Sadio Mane NA Virgil van Dijk wameingia kwenye orodha ya wachezaji 30 wanaowania tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia, Ballon d'Or iliyotangazwa Ufaransa jana.  
    Mane na Van Dijk ni miongoni mwa wachezaji saba wa Liverpool katika orodha hiyo ambao wanaungana na nyota wengine wa Ligi Kuu ya England, Sergio Aguero, Bernardo Silva na Pierre-Emerick Aubameyang. 
    Wachezaji wengine wa Liverpool ni Salah, Roberto Firmino, Alisson, Georginio Wijnaldum na Trent Alexander-Arnold ambao wote walikuwemo kwenye kikosi cha timu hiyo kilichotwaa taji la saba la Ligi ya Mabingwa. 
    Ronaldo na Messi wote watakuwa wakiwania tuzo ya sita ya Ballon d'Or, wawili hao wakitarajiwa kuchuana tena msimu huu, huku mshindi wa tuzo hiyo mwaka jana,  Luka Modric akikosekana kwenye orodha hiyo ya watu 30.
    Beki Virgil van Dijk wa Liverpool na Uholanzi ameteuliwa kuwania tuzo ya Ballon d'Or mwaka huu 


    NYOTA 30 WANAOWANIA BALLON D'OR

    Sadio Mane - Liverpool
    Sergio Aguero - Manchester City 
    Frenkie de Jong - Ajax/ Barcelona 
    Hugo Lloris - Tottenham 
    Dusan Tadic - Ajax
    Kylian Mbappe - PSG
    Trent Alexander-Arnold - Liverpool
    Donny van de Beek - Ajax
    Pierre-Emerick Aubameyang - Arsenal
    Marc-Andre Ter-Stegen - Barcelona 
    Cristiano Ronaldo - Juventus
    Alisson - Liverpool
    Matthijs de Ligt - Juventus
    Karim Benzema - Real Madrid
    Georginio Wijnaldum - Liverpool
    Virgil van Dijk - Liverpool
    Bernardo Silva - Manchester City
    Heung-min Son - Tottenham Hotspur
    Robert Lewandowski - Bayern Munich
    Roberto Firmino - Liverpool
    Lionel Messi - Barcelona
    Kevin de Bruyne - Manchester City
    Kalidou Koulibaly - Napoli
    Riyad Mahrez - Manchester City
    Antoine Griezmann - Barcelona 
    Mohamed Salah - Liverpool
    Joao Felix - Atletico Madrid
    Eden Hazard - Real Madrid
    Marquinhos - PSG


























    Raheem Sterling - Man City 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: VAN DIJK KUPAMBANA NA MESSI NA RONALDO KUWANIA BALLON D'OR Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top