Mshambuliaji Gareth Bale akikimbia kushangilia baada ya kuifungia Real Madrid bao la tatu dakika ya 74 katika ushindi wa 3-1 dhidi ya wenyeji Atletico Madrid Uwanja wa Wanda Metropolitano mjini Madrid kufuatia kutokea benchi dakika ya 57 kuchukua nafasi ya Vinicius Junior, hilo likiwa bao lake la 100 tangu ajiunge na klabu hiyo. Mabao mengine ya Real Madrid yamefungwa na Casemiro dakika ya 16 na Sergio Ramos dakika ya 42 kwa penalti wakati la Atletico Madrid limefungwa na Antoine Griezmann dakika ya 25 katika mchezo ambao wenyeji walimaliza pungufu baada ya kiungo wao, Thomas Partey kutolewa kwa kadi nyekundu kufuatia kuonyeshwa kadi ya pili ya njano. Kwa ushindi huo, Real Madrid inafikisha pointi 45 katika mechi ya 23 na kupanda hadi nafasi ya pili, ikiizidi kwa pointi moja Atletico Madrid na ikizidiwa kwa pointi tano na vinara, Barcelona ambao pia wamecheza mechi 22 na watamenyana na Athletic Club PICHA ZAIDI GONGA HAPA
Liverpool are 'set to lose another key staff member at the end of the
season' - with coach joining Jurgen Klopp and others in leaving Anfield
-
Liverpool are set to lose another key member of the club's coaching
department at the end of the season as Jurgen Klopp confirmed his plans to
leave Anfiel...
8 minutes ago
0 comments:
Post a Comment