Marco Asensio akishangilia baada ya kuifungia Real Madrid bao la ushindi dakika ya 87 katika ushindi wa 2-1 dhidi ya wenyeji, Ajax kwenye mchezo wa kwanza wa hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa jana Uwanja wa Johan Cruijff Arena mjini Amsterdam. Real Madrid walitangulia kwa bao la Karim Benzema dakika ya 60 akimalizia kazi nzuri ya Vinicius Junior, kabla ya Ajax kusawazisha kupitia kwa Hakim Ziyech dakika ya 74 akimalizia pasi ya David Neres na kupata bao la pili lililofungwa na Nicolas Tagliafico akitumia makosa ya kipa Thibaut Courtois, lakini bao likakataliwa baada ya refa Damir Skomina kupata msaada wa marudio ya picha za video (VAR) PICHA ZAIDI GONGA HAPA
Children to be banned from using phones in schools in England by law
-
The British government said it will pass legislation to bar smartphones
from schools in England amid a broader battle over whether to ban social
media.
1 hour ago



.png)
0 comments:
Post a Comment