Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
KIPA wa Simba SC, Ivo Mapunda amewasili Afrika Kusini na leo amefanyiwa vipimo ambayo vimeonyesha anaweza kuanza mazoezi magumu kuelekea mchezo wa watani wa jadi, Yanga SC Jumamosi wiki hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kipa huyo wa kwanza wa Wekundu wa Msimbazi aliumia kidole wiki ya mwisho ya Septemba mwaka huu akiwa mazoezini na timu yake visiwani, Zanzibar na akatakiwa kuwa nje kwa wiki nane.
Hata hivyo, tiba nzuri aliyopatiwa imepunguza muda wa kuwa nje kwa mzuia michomo huyo na anaweza kuwa tayari kurudi uwanjani baada ya wiki sita.
Ivo amewasili jana na wachezaji waliokuwa kwenye kikosi cha timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, mabeki Miraji Adam na Joram Mgeveke na viungo Jonas Mkude, Amri Kiemba, Said Ndemla na Haruna Chanongo.
Mshambuliaji Mganda, Emmanuel Okwi anatarajiwa kuwasili usiku wa leo baada ya kuichezea Uganda, The Cranes Jumamosi katika mechi ya kufuzu AFCON.
Simba SC ilikuwa icheze na Jomo Cosmos leo, lakini mchezo huo umesogezwa hadi kesho kwa sababu mechi dhidi ya SuperSport United iliyokuwa ifanyike kesho imefutwa.
Simba SC inaendelea vizuri na maandalizi yake, ikiwa imeweka kambi katika Eden Vale PETRA na ikijifua mara mbili kwa siku katika viwanja vya hoteli hiyo.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili wa Simba SC, Kassim Mohamed Dewji amekwenda kuongeza nguvu Afrika Kusini akiungana na Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano, Mohammed Nassor ‘Steven Seagal’ na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji, Collins Frisch na Said Tuliy.
Simba SC imecheza mechi mbili Afrika Kusini ambako ilitua wiki iliyopita na mchezo wa kwanza ilitoa sare ya 0-0 na Orlando Pirates kabla ya kufungwa 4-2 na Bidvest Wits, au Wits University.
Katika mchezo na Pirates kipa, Hussein Sharrif ‘Cassilas’ aliumia na kocha Patrick Phiri akaamua kumpumzisha tangu hapo, akimtumia kipa wa tatu, Peter Manyika.
Lakini taarifa zinasema Cassilas anaendelea vizuri na Mapunda naye amewasili Afrika Kusini kuongeza nguvu.
KIPA wa Simba SC, Ivo Mapunda amewasili Afrika Kusini na leo amefanyiwa vipimo ambayo vimeonyesha anaweza kuanza mazoezi magumu kuelekea mchezo wa watani wa jadi, Yanga SC Jumamosi wiki hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kipa huyo wa kwanza wa Wekundu wa Msimbazi aliumia kidole wiki ya mwisho ya Septemba mwaka huu akiwa mazoezini na timu yake visiwani, Zanzibar na akatakiwa kuwa nje kwa wiki nane.
Hata hivyo, tiba nzuri aliyopatiwa imepunguza muda wa kuwa nje kwa mzuia michomo huyo na anaweza kuwa tayari kurudi uwanjani baada ya wiki sita.
![]() |
| Kipa Ivo Mapunda amewasili Afrika Kusini na kufanyiwa vipimo ambavyo vimeonyesha anaweza kuanza mazoezi |
Ivo amewasili jana na wachezaji waliokuwa kwenye kikosi cha timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, mabeki Miraji Adam na Joram Mgeveke na viungo Jonas Mkude, Amri Kiemba, Said Ndemla na Haruna Chanongo.
Mshambuliaji Mganda, Emmanuel Okwi anatarajiwa kuwasili usiku wa leo baada ya kuichezea Uganda, The Cranes Jumamosi katika mechi ya kufuzu AFCON.
Simba SC ilikuwa icheze na Jomo Cosmos leo, lakini mchezo huo umesogezwa hadi kesho kwa sababu mechi dhidi ya SuperSport United iliyokuwa ifanyike kesho imefutwa.
Simba SC inaendelea vizuri na maandalizi yake, ikiwa imeweka kambi katika Eden Vale PETRA na ikijifua mara mbili kwa siku katika viwanja vya hoteli hiyo.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili wa Simba SC, Kassim Mohamed Dewji amekwenda kuongeza nguvu Afrika Kusini akiungana na Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano, Mohammed Nassor ‘Steven Seagal’ na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji, Collins Frisch na Said Tuliy.
Simba SC imecheza mechi mbili Afrika Kusini ambako ilitua wiki iliyopita na mchezo wa kwanza ilitoa sare ya 0-0 na Orlando Pirates kabla ya kufungwa 4-2 na Bidvest Wits, au Wits University.
Katika mchezo na Pirates kipa, Hussein Sharrif ‘Cassilas’ aliumia na kocha Patrick Phiri akaamua kumpumzisha tangu hapo, akimtumia kipa wa tatu, Peter Manyika.
Lakini taarifa zinasema Cassilas anaendelea vizuri na Mapunda naye amewasili Afrika Kusini kuongeza nguvu.



.png)
0 comments:
Post a Comment