• HABARI MPYA

    Thursday, November 14, 2013

    UWANJA WA KARUME NI HATARI KWA MAISHA YA WACHEZAJI STARS, LAKINI SUTI MOJA TU YA TENGA AU MALINZI INAWEZA KUEPUSHA MAJANGA

    Nyavu za magoli ya Uwanja wa Karume zimechakaa na zinapofugwa zinashikiziwa kwa mawe, kitu ambacho ni hatari kwa usalama wa wachezaji. Mchezaji anaweza kuumia vibaya akiangukia kwa kishindo kikubwa moja ya mawe yaliyowekwa kwenye lango. Hii ni fedheha kwa nchi yetu, Uwanja huu ndio ambao timu zetu za taifa zinafanya mazoezi, lakini viongozi waliomaliza muda wao, chini ya Rais Leodegar Tenga hawakuliona hili na hawa walioingia madarakani chini ya Rais Jamal Malinzi pia hawajaliona hili. Je, wanasubiri siku mchezaji apasuliwe kichwa na mawe haya ndiyo wachukue hatua. Suti moja ya Tenga au Malinzi ingeweza kununua nyavu nzuri za kuweka kwenye magoli ya Karume na chenji wangerudishiwa, au na hili pia tunasubiri msaada wa FIFA?
    Kipa Ivo Mapunda alihatarisha maisha yake jana angalia ma
    we hayo chini

    Suti moja tu ya Malinzi kulia au Tenga kushoto inaweza kununua nyavu nzuri Karume
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: UWANJA WA KARUME NI HATARI KWA MAISHA YA WACHEZAJI STARS, LAKINI SUTI MOJA TU YA TENGA AU MALINZI INAWEZA KUEPUSHA MAJANGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top