NYASI za Uwanja wa Estadio da Luz mjini Lisbon, Ureno zitawaka moto leo kwa mpambano baina ya wenyeji dhidi ya Sweden kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia mwakani Brazil.
Huo utakuwa mchezo wa kwanza wa mchujo na wa pili utachezwa mjini Stockholm, Sweden Jumanne ijayo, ambako mshindi wa matokeo ya jumla ndiye atakayekwenda Brazil. Ni mechi ambayo itawakutanisha wachezaji wawili maarufu duniani, Cristiano Ronaldo wa Ureno na Zlatan Ibrahimovic wa Sweden.
Wazi nyota kweli ni yule ambaye ataiasaidia timu yake kupata tiketi ya kwenda Brazil.
Mpira mguuni: Zlatan Ibrahimovic akimiliki mpira katika mazoezi ya Sweden kujiandaa kuivaa Ureno
"Zlatan kwangu ni namba moja duniani," amesema kocha wa Sweden, Erik Hamren jana usiku baada ya kutua Ureno.
"Ni mchezaji wa kiwango cha dunia, ni hodha wangu na anachezea Sweden. Nasema kwamba ni bora sana.".
Wakati huo huo, mchezaji mwenzake Ronaldo, Pepe ametoa maoni yake katika mjadala huo. "Wao ni wachezaji wawili wakubwa, lakini hakuna cha kufananisha na anachokifanya Cristiano," alisema beki huyo wa Real Madrid. "Ana takwimu ambazo kufikiria na ni bora duniani. Hakuna cha kufananisha,".
Vita ya meneno: Beki wa Ureno, Pepe (kushoto) na kocha wa Sweden, Erik Hamren wametoa maoni tofauti kuhusu wawili hao
Ronaldo akiwa na kocha Paulo Bento baada ya kukosa penalti katika Euro 2012 dhidi ya Hispania
Ibrahimovic amebeba matumaini ya Sweden mabegani mwake
Wote Ronaldo (kushoto) na Ibrahimovic wanaingia kwenyemechi hiyo wakiwa wapo vizuri na wametoka kuzibeba klabu zao
Lakini nani atakosa Fainali za Kombe la Dunia kati yao?
Ronaldo au Ibrahimovic? Jibu kamili litapatikana Jumanne ijayo Stockholm.



.png)
0 comments:
Post a Comment