KLABU ya Arsenal imepewa ofa ya kumsajili Salomon Kalou ifikapo Januari.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Chelsea, kwa sasa anachezea klabu ya Lille ya Ufaransa, na yupo tayari kurejea Ligi Kuu England katika dirisha dogo.
Na Kalou, anaweza kutolewa kwa dau la Pauni Milioni 2.5 amewaelekeza washauri wake kufutilia timu zinazomtaka England kuelekea Januari.
Bluu: Juan Mata (juu) akimpongea Kalou baada ya kuifungia bao Chelsea dhidi ya Benfica katika Ligi ya Mabingwa
Arsenal ni miongoni mwa klabu ambazo zimekuwa zikimmezea mate nyota huyo wa kimataifa wa Ivory Coast kwa wiki za karibuni.
Na kama inavyofahamika The Gunners wapo sokoni kusaka mshambuliaji, basi milango iko wazi kwao.
Kocha Arsene Wenger anataka kusajili mshambuliaji wa kusaidiana na mshambuliaji wake pekee wa sasa, Mfaransa Olivier Giroud, na bila shaka Kalou atafaa.
Arsenal ilikaribia kumsajili Kalou Januari 2012, lakini mshambuliaji huyo alikataa baada ya kuambiwa atapunguziwa mshahara hadi Pauni 20,000 kwa wiki kutoka 60,000 alizokuwa akilipwa Stamford Bridge.
Kocha wa West Bromwich, Steve Clarke pia alitaka kumsajili Kalou mwanzoni mwa msimu huu, lakini mchezaji mwenye kasi aliyezaliwa miaka 28 iliyopita akaamua kubaki Ufaransa.
Anahitaji: Wenger (juu) anahitaji mshambuliaji mwingine Arsenal
Namba 1: Arsenal iko hatarini kwa sababu ina mshambuliaji mmoja tu, Olivier Giroud ambaye akiumia klabu itabaki bila mshambuliaji



.png)
0 comments:
Post a Comment