• HABARI MPYA

    Thursday, September 17, 2020

    PARIS SAINT-GERMAIN YAPATA USHINDI WA KWANZA LIGUE 1

    MABINGWA watetezi, Paris Saint-Germain jana wamepata ushindi wa kwanza katika Ligue 1 baada ya kuichapa FC Metz 1-0, bao pekee la kiungo Mjerumani, Julian Draxler dakika ya 90 na ushei Uwanja wa Parc des Princes Jijini Paris.

    PSG ilimaliza pungufu baada ya Abdou Diallo kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 65. Ikumbukwe,  mechi mbili za mwanzo PSG walifungwa 1-0 mara mbili na Lens na Marseille.

    Winga Mjerumani, Julian Draxler akishangilia baada ya kuifungia Paris Saint-Germain jbao pekee katika ushindi wa 1-0 dhidi ya FC Metz jana PICHA ZAIDI GONGA HAPA 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: PARIS SAINT-GERMAIN YAPATA USHINDI WA KWANZA LIGUE 1 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top