• HABARI MPYA

    Wednesday, January 29, 2020

    MTENDAJI MKUU WA AZAM FC AFANYA ZIARA KLABU KADHAA NCHINI MISRI, AKUTANA HADI NA HIMID MAO

    OFISA Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Abdulkarim Amin 'Popat', akiwa makao makuu ya miamba ya soka barani Afrika, Al Ahly.
    Popat amefanya ziara hiyo leo, kwa lengo kuu la kujifunza mambo mbalimbali ya soka, pamoja na kujionea uwekezaji uliofanywa na klabu hiyo ya karne barani Afrika.
    Aidha kwenye ziara hiyo alikuwa sambamba na mwenyeji wake, Amgad Alghoniny, ambaye ni Mhariri wa kitengo cha habari cha timu hiyo.
    Mbali ya kutembelea kwa miamba hiyo, Popat pia alipata fursa ya kukutana na Nahodha wa zamani wa Azam FC, Himid Mao 'Ninja', anayekipiga nchini humo katika timu ya ENPPI. 
    Hapa akiwa na kiungo wa zamani wa Azam FC, Mtanzania Himid Mao ambaye kwa sasa anachezea ENPPI 
    Hapa akiwa na Himid Mao na mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi, Fiston Abdul Razak anayecheza naye ENPPI 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MTENDAJI MKUU WA AZAM FC AFANYA ZIARA KLABU KADHAA NCHINI MISRI, AKUTANA HADI NA HIMID MAO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top