Mshambuliaji kinda Mbrazil, Rodrygo Silva de Goes akishangilia baada ya kuifungia Real Madrid mabao matatu dakika ya nne, saba na 90 na ushei katika ushindi wa 6-0 dhidi ya Galatasaray kwenye mchezo wa Kundi A Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa Jumatano Uwanja wa Bernabeu. Mabao mengine ya Real yamefungwa na Sergio Ramos kwa penalti dakika ya 14, Karim Benzema dakika ya 45 na 81 na kwa ushindi huo, timu ya kocha Mfaransa Zinadine Zidane inafikisha pointi saba, ikiendelea kushika nafasi ya pili ikizidiwa pointi tano na vinara Paris Saint-Germain baada ya timu zote kucheza mechi nne PICHA ZAIDI GONGA HAPA
Trump will welcome Iran at World Cup - Infantino
-
US President Donald Trump has said Iran are "welcome" to take part in this
summer's World Cup despite the countries being at war, according to Fifa
preside...
1 hour ago



.png)
0 comments:
Post a Comment