• HABARI MPYA

    Sunday, May 10, 2015

    KOMBE LA KAGAME KUANZA JULAI 11 DAR, TFF YAKUBALI UENYEJI

    Yanga SC walikuwa mabingwa michuano hiyo ilipofanyika mara ya mwisho mwaka 2012
    SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), leo hii imekubali kuwa wenyeji wa  michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, maarufu kama Kombe la Kagame.
    Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati, CECAFA ambao ndio wamiliki wa mashindano haya watatoa mialiko kwa klabu zenye sifa ya kushiriki na wakipokea uthibitisho wa ushiriki wao watatoa orodha ya klabu shiriki na ratiba ya michuano hiyo.
    Michuano hii inatarajiwa kuafanyika nchini kuanzia Julai 11 hadi Agosti 2, mwaka 2015.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KOMBE LA KAGAME KUANZA JULAI 11 DAR, TFF YAKUBALI UENYEJI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top