• HABARI MPYA

    Tuesday, May 26, 2015

    REAL MADRID YAMFUKUZA KAZI ANCELOTTI BAADA YA KUMALIZA MSIMU BILA TAJI

    KLABU ya Real Madrid imemfukuza kocha Carlo Ancelotti mwaka mmoja na siku moja tangu aipe timu hiyo taji la 10 la Ulaya.
    Rais wa klabu, Florentino Perez amethibitisha katika Mkutano na Waandishi wa Habari usiku wa Jumatatu juu ya uamuzi wa kumtimua kocha huyo wa tisa katika miaka yake 12 ya kuwa madarakani, Lakini akazuiwa kwa muda kumtaja Rafa Benitez kuwa kocha mpya.
    Kocha huyo wa zamani wa Liverpool anabaki kuwa mwenye nafasi kubwa ya kurithi mikoba ya Ancelotti ambaye kufukuzwa kwake hakujawafurahisha wahezaji na mashabiki.
    Carlo Ancelotti has been sacked by Real Madrid after overseeing a trophyless season at the Bernabeu
    Carlo Ancelotti amefukuzwa Real Madrid baada ya kumaliza msimu bila taji
    Real Madrid president Florentino Perez announced on Monday evening that Ancelotti had been sacked

    Rais wa Real Madrid, Florentino Perez ametangaza kumfukuza Ancelotti 

    MAKOCHA TISA ALIOFUKUZA FLORENTINO PEREZ NDANI YA MIAKA 12 

    Vicente del Bosque (Juni 23, 2003)
    Carlos Queiroz (Mei 24, 2004)
    Jose Antonio Camacho (Septemba 20, 2004)
    Marino Garia Remon (Desemba 30, 2004)
    Vanderlei Luxemburgo (Desemba 4, 2005)
    Fabio Capello (Juni 28, 2007)
    Bernd Schuster (Desemba 9, 2008)
    Manuel Pellegrini (Mei 26, 2010)
    Carlo Ancelotti (Mei 25, 2014)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: REAL MADRID YAMFUKUZA KAZI ANCELOTTI BAADA YA KUMALIZA MSIMU BILA TAJI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top