• HABARI MPYA

    Sunday, May 10, 2015

    BALE ANASOTA REAL MADRID KWA SABABU WENZAKE HAWAMPI PASI, ALALAMA WAKALA WAKE

    WAKALA Jonathan Barnett wa mchezaji Gareth Bale amesema kijana wake anasota Real Madrid kwa sababu wachezaji wenzake hawampi pasi za kutosha.
    Lakini Barnett amesema winga huyo wa kimataifa wa Wales hana mpango wa kuondoka katika klabu hiyo.
    Bale amejikuta katika msimu wa pili mgumu Hispania Jumanne tu iliyopita akitoka kucheza kwa kiwango cha chini Real ikifungwa na Juventus 2-1 na Jumamosi akashindwa kuisaidia timu yake hiyo ikilazimishwa sare ya 2-2 na Valencia katika La Liga.
    Tayari ameanza kuzongwa na kuzomewa na mashabiki Uwanja wa Bernabeu, licha ya kwamba alifunga mabao katika fainali za Ligi ya Mabingwa na Kombe la Mfalme msimu uliopita Rea ikitwaa mataji yote hayo.
    Gareth Bale's agent has put his client's drop in form down to his team-mates' failure to pass him the ball

    Real ilivunja rekodi ya usajili wa 'bei mbaya' kumsajili nyota huyo mwenye umri wa miaka 25, lakini wameshindwa kupata walichokitarajia kutokana na mchezaji huyo kuandamwa na majeruhi.
    "Real wanatakiwa kufanya kazi na Gareth na kumpasia mipira zaidi,"amesema wakala wa Bale, Jonathan Barnett.
    "Mpe mipira zaidi na acha amuonyeshe kila mmoja uzuri wake. Atakuwa mchezaji bora Real Madrid wakati wachezaji wenzake watakapoanza kushirikiana naye na kumsaidia," amesema.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BALE ANASOTA REAL MADRID KWA SABABU WENZAKE HAWAMPI PASI, ALALAMA WAKALA WAKE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top