TIMU ya KMC imelazimishwa sare ya bila mabao na Kagera Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Jijini Dar es Salaam.
Kwa matokeo hayo, KMC inafikisha pointi 33 katika mchezo wa 25 ingawa na inabaki nafasi ya tano ikizidiwa tu wastani wa mabao Coastal Unión ambayo pia ina mechi moja mkononi.
Kwa upande wao Kagera Sugar wanafikisha pointi 30 katika mchezo wa 25 nafasi ya saba.
0 comments:
Post a Comment