WENYEJI, Manchester United jana wamelazimishwa sare ya 1-1 na AC Milan katika mchezo wa kwanza Hatua ya 32 Bora UEFA Europa League Uwanja wa Old Trafford Jijini Manchester.
Mshambuliaji kinda wa umri wa miaka 18, Muivory Coast, Amad Diallo alianza kuifungia Man United dakika ya 50 akimalizia pasi ya Bruno Fernandes, kabla ya beki mkongwe, Mdenmark Simon Thorup Kjaer kuisawazishia AC Milan dakika ya 90 na ushei akimalizia pasi ya kiungo Rade Krunic na timu hizo zitarudiana Machi 18 Uwanja wa Giuseppe Meazza Jijini Milan PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment