Barcelona imefanikiwa kwenda fainali ya Kombe la Mfalme, Ufaransa baada ya ushindi wa 3-0 dhidi ya Sevilla jana, mabao ya Ousmane Dembele, Gerard Pique na Martin Braithwaite Uwanja wa Camp Nou.
Kwa matokeo hayo, Barcelona inatinga fainali kwa ushindi wa jumla wa 3-2 baada ya kufungwa 2-0 kwenye mchezo wa kwanza wa Nusu Fainali mwezi Februari.
Sevilla ilipoteza nafasi nzuri ya kupata bao baada ya mkwaju wa penalti wa Lucas Ocampos kuokolewa na Marc-Andre ter Stegen na sasa Barce itakutana na mshindi kati ya Athletic Bilbao na Levante katika fainali PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment