NAHODHA, Lionel Messi jana amefunga mabao mawili dakika ya 13 na 90 Barcelona ikiichapa Huesca 4-1 katika mchezowa LaLiga Uwanja wa Camp Nou, huku Muargentina huyo mwenye umri wa miaka 33 akifikia rekodi ya Xavi ya kuichezea timu hiyo mechi 767.
Mabao mengine ya Barcelona yalifungwa na Antoine Griezmann dakika ya 35 na Oscar Mingueza dakika ya 53, wakati la Huesca lilifungwa Rafa Mir dakika ya 45 kwa penalti na kwa ushindi huo timu ya Katalunya inazidiwa pointi nne na vinara, Atletico Madrid PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment