• HABARI MPYA

    Friday, February 28, 2020

    FRED APIGA MBILI MAN UNITED YASHINDA 5-0 EUROPA LEAGUE

    Kiungo wa Manchester United, Frederico Rodrigues Santos 'Fred' akishangilia baada ya kuifungia mabao mawili timu hiyo dakika za 82 na 90 katika ushindi wa 5-0 Uwanja wa Old Trafford usiku wa jana dhidi ya Club Brugge KV kwenye mchezo wa marudiano Hatua ya 32 Bora UEAFA Europa League. Mabao mengine ya Manchester United yalifungwa na Bruno Fernandes kwa penalti dakika ya 27, Odion Ighalo dakika ya 34 na Scott McTominay dakika ya 41 na kwa ushindi huo Mashetani Wekundu wanatinga 16 Bora kwa ushindi wa jumla wa 6-1 baada ya sare ya 1-1 kwenye mchezo wa kwanza Ubelgiji 


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: FRED APIGA MBILI MAN UNITED YASHINDA 5-0 EUROPA LEAGUE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top