• HABARI MPYA

    Thursday, February 08, 2018

    SIMBA SC NA AZAM FC KATIKA PICHA JANA CHAMAZI

    Mshambuliaji wa Simba, Mganda Emmanuel Okwi akimtoka kiungo wa ulinzi wa Azam FC, Mcameroon Daniel Amoah katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Simba ilishinda 1-0 
    Nahodha wa Simba SC, John Bocco akiteleza kuondosha mpira miguuni mwa beki wa Azam, Mghana Daniel Amoah  
    Kipa wa Simba SC, Aishi Salum Manula akiwa juu kudaka mpira kiulaini, huku mabeki wake Shomary Kapombe na James Kotei wakiwa tayari kumsaidia dhidi ya mshambuliaji wa Azam, Shaaban Iddi Chilunda 
    Kiungo wa Simba, Said Hamisi Ndemla akimtoka winga Mghana wa Azam FC, Enock Attta-Agyei
    Shaaban Iddi Chilunda wa Azam FC akikosa bao la wazi 
    Beki wa Azam FC, Aggrey Morris akimiliki mpira mbele ya kiungo wa Simba, Jonas Mkude 
    Kiungo wa Azam, Salum Abubakar 'Sure Boy' akiondoka na mpira mbele ya Simba, Muzamil Yassin  
    Mshambuliaji wa Azam, Mghana Bernard Arthur akiwatoka mabeki wa Simba
    Kikosi cha Azam FC kabla ya mchezo wa jana
    Kikosi cha Simba SC kabla ya mchezo wa jana Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA SC NA AZAM FC KATIKA PICHA JANA CHAMAZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top