• HABARI MPYA

    Thursday, May 14, 2015

    MANJI AAMBIWA; “UMEMALIZA MUDA WAKO YANGA SC”, KAMATI YAITISHA UCHAGZUI JULAI 12 DAR

    Na Prince Akbar, DAR ES SALAAM 
    UCHAGUZI Mkuu wa Yanga SC utafanyika Julai 12, mwaka huu katika ukumbi ambao utatajwa baadaye.
    Taarifa ya Katibu Kamati ya Uchaguzi ya Yanga SC, Francis Kaswahili iliyotumwa BIN ZUBEIRY leo imesema kwamba, fomu za wagombea zitaanza kutolewa Mei 17, mwaka huu kwa kuzingatia ratiba.
    “Jambo hili ni la kikatiba na wala halina mjadala, tunataka Yanga iwe na viongozi ambao watatokana na utashi wa Wanayanga ni matumaini ya kamati ya uchaguzi kwamba hapatatoka mtu mwingine wa kutaka kuvunja misingi ya katiba.
    Mwenyekiti wa Yanga SC, Yussuf Manji ameambiwa amemaliza muda wake madarakani

    “Huu ni utamaduni wa mwanadamu anayeishi katika mfumo wa demokrasia na hasa ikizingatiwa kwamba mwaka 2015 ni mwaka pia wa uchaguzi, wa Rais , Wabunge na Madiwani,”amesema Kaswahili. 
    Ameongeza kwamba, lengo ni mwendelezo wa kupokezana vijiti na kwamba kiongozi bora atapatikana kwa misingi bora ya kikatiba na si vinginevyo.
    Itakumbukwa kwamba kwa mara ya mwisho Yanga SC ilifanya uchaguzi wake Julai 18, mwaka 2010 na Wakili Lloyd Biharangu Nchunga alichaguliwa kuwa Mwenyekiti, Makamu wake, Devis Mosha na Wajumbe; Charles Mgondo, Ally Mayayi Tembele, Mzee Yussuf, Theonest Rutashobolwa (marehemu), Titus Ossoro, Sara Ramadhani, Mohamed Bhinda na Salum rupia. 
    Hata hivyo, kwa vipindi tofauti baadhi ya viongozi walijiuzulu nyadhifa zao na hivyo ikalazimika kufanyika uchaguzi mdogo ufanyike Julai 15, mwaka 2012 na Yussuf Manji alichaguliwa kuwa Mwenyekiti, Makamu wake Clement Sanga na Wajumbe; Aaron Nyanda, George Manyama, Abdallah Bin Kleb na Mussa Kutabaro. 
    “Na itakumbukwa kamba wale wote ambao waliingia kwa kuziba nafasi wzi walikuwa wanatumikia mhula ulioanza tarehe 18/07/2010 na ulikoma tarehe 17/07/2014 na hivyo viongozi wote nafasi zao kwa sasa zipo wazi,”amesema Kaswahili.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MANJI AAMBIWA; “UMEMALIZA MUDA WAKO YANGA SC”, KAMATI YAITISHA UCHAGZUI JULAI 12 DAR Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top