• HABARI MPYA

    Friday, February 27, 2015

    LIVERPOOL YATUPWA NJE YA MICHUANO YA ULAYA

    LIVERPOOL imetupwa nje ya michuano ya Europa League, baada ya kufungwa kwa penalti 5-4 na Besiktas kufuatia sare ya jula ya 1-1.
    Tolgay Arslan alitokea benchi na kuifungia Besiktas bao dakika ya 72 Uwanja wa Ataturk, Istanbul nchini Uturuki akimalizia ‘pande’ la Demba Ba na kufanya sare ya jumla ya 1-1 baada ya Liverpool kushinda 1-0 katika mchezo wa kwanza England.
    Ba angeweza kufunga bao la ushindi dakika ya  92, kama asingegongesha mwamba akiwa umbali wa mita sita.
    Baada ya dakika 120, penalti za Besiktas zilifungwa na Ba, Lambert, Tore, Lallana na Kavlak, wakati zilifungwa na Can, Hutchinson, Allen na Arslan huku Lovren akikosa.
    Kikosi cha Besiktas kilikuwa; Gonen, Opare, Franco, Uysal, Kurtulus, Hutchinson, Kavlak, Tore, Sosa/Arslan dk61, Sahan/Frei dk105 na Ba.
    Liverpool: Mignolet, Toure, Lovren, Skrtel, Moreno, Can, Allen, Sterling, Ibe/Manquillo dk76, Sturridge/Lambert dk106 na Balotelli/Lallana dk82.
    Liverpool failed to repeat their 2005 Champions League final heroics in Istanbul as they were dumped out of the Europa League by Besiktas
    Wachezaji wa Liverpool wakisitika baada ya kutolewa Europa League na Besiktas, kulia Demba Ba akishangilia

    PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2970765/Besiktas-1-0-Liverpool-agg-1-1-AET-Reds-fail-repeat-2005-Champions-League-heroics-Istanbul-crash-Europa-League-round-32-penalties-Dejan-Lovren-s-miss.html#ixzz3StRdUQrn 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LIVERPOOL YATUPWA NJE YA MICHUANO YA ULAYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top