Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
KIKOSI kamili cha Yanga kinakwea pipa Jumatano alfajiri kuelekea Botsawna tayari kwa mchezo wa marudiano dhidi ya BDF XI ya huko.
Katibu wa Yanga Dk Jonas Tiboroha amesema kikosi chao kitaondoka na wachezaji wote watakaopitishwa na kocha wao Hans Pluijm ambaye kesho atataja idadi kamili ya msafara wao.
Tibohora ambaye pia kitaaluma ni kocha amesema kikosi chao kitaondoka na Ndege ya Shirika la Kenya tayari kwa mchezo huo wa kombe la Shirikisho utakaopigwa Ijumaa nchini humo ambapo Yanga itarejea Jumapili baada ya mchezo huo.
"Tunatarajia kuondoka hapa Jumatano keshokutwa kuelekea Botswana,kwasasa tunasubiri kocha na timu irejee leo ikitokea Mbeya na baada ya hapo tutamalizia maandalizi ya safari yetu,"amesema Tiboroha.
KIKOSI kamili cha Yanga kinakwea pipa Jumatano alfajiri kuelekea Botsawna tayari kwa mchezo wa marudiano dhidi ya BDF XI ya huko.
Katibu wa Yanga Dk Jonas Tiboroha amesema kikosi chao kitaondoka na wachezaji wote watakaopitishwa na kocha wao Hans Pluijm ambaye kesho atataja idadi kamili ya msafara wao.
Tibohora ambaye pia kitaaluma ni kocha amesema kikosi chao kitaondoka na Ndege ya Shirika la Kenya tayari kwa mchezo huo wa kombe la Shirikisho utakaopigwa Ijumaa nchini humo ambapo Yanga itarejea Jumapili baada ya mchezo huo.
"Tunatarajia kuondoka hapa Jumatano keshokutwa kuelekea Botswana,kwasasa tunasubiri kocha na timu irejee leo ikitokea Mbeya na baada ya hapo tutamalizia maandalizi ya safari yetu,"amesema Tiboroha.
0 comments:
Post a Comment