• HABARI MPYA

    Monday, February 23, 2015

    JULIO ALIANZISHA MAPEMAAA, ASAKA WAKANDIAJI WA ‘VIBABU VYAKE’

    Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
    KOCHA Mkuu wa Mwadui ambayo jana ailitwaa 'mwali' wa ubingwa wa Ligi Daraja la kwanza Jamhuri Kihwelo 'Julio' amefurahia mafanikio hayo kwa kuwasaka wale wote waliokuwa wakimbeza kwa kuwaita wakongwe.
    Akizungumza na BIN ZUBEIRY, Julio amesema alikuwa anajua nini anakitaka kwa wachezaji wakongwe wakiongozwa na viungo Athuman Idd 'Chuji', Uhuru Seleman, Julius Mrope, mshambuliaji Monja Liseki na mabeki Juma Jabu na Said Sued.
    Kocha wa Mwadui FC ya Shinyanga ameanza kutamba baada ya kupanda Ligi Kuu

    Julio amesema uzoefu wa wachezaji hao ndiyo umesaidia kupatakana kwa mafanikio hayo ambapo nyota hao walikuwa wanazingatia mafundisho yake.
    "Nilikuwa nawashangaa wote waliokuwa wananiona mimi mjinga kwa kuwaita hawa ndiyo maana wakati tunashangilia pale uliona vijana wangu wakiimba hayo maneno ya wazee,alisema Julio.
    "Nilijua nataka nini kwao,mimi ni kocha wa mpira kuna wakati lazima watu watuachie walimu kazi yetu tuifanye bila kuingiliwa wakongwe hawa waliokuwa wanaonekana wazee ndiyo sasa wametupa kombe.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: JULIO ALIANZISHA MAPEMAAA, ASAKA WAKANDIAJI WA ‘VIBABU VYAKE’ Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top