• HABARI MPYA

    Monday, November 03, 2014

    RANGERS YAPUNGUZWA KASI MBIO ZA LIGI KUU 2015

    Friends Rangers (pichani) imetoka sare ya kufungana bao 1-1 na Polisi Dar es Salaam katika mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Karume, Dar es Salaam. Magige Bellence alitangulia kuifungia Polisi dakika ya 67, kabla ya Friends kusawazisha dakika ya 88 kupitia kwa Almasi Mkinda, aliyefunga kwa penalti, baada ya Salmin Mohamed kuunawa mpira. Friends inatimiza pointi 12 sawa na Majimaji ya Songea inayoongoza Kundi A.   

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RANGERS YAPUNGUZWA KASI MBIO ZA LIGI KUU 2015 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top