// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); SUAREZ AANZA KUPIGA MZIGO LEO BARCA NA KUSEMA; "NAJISIKIA FURAHA KUWA MCHEZAJI TENA" - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE SUAREZ AANZA KUPIGA MZIGO LEO BARCA NA KUSEMA; "NAJISIKIA FURAHA KUWA MCHEZAJI TENA" - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Friday, August 15, 2014

    SUAREZ AANZA KUPIGA MZIGO LEO BARCA NA KUSEMA; "NAJISIKIA FURAHA KUWA MCHEZAJI TENA"

    MSHAMBULIAJI Luis Suarez ameelezea furaha yake ya kuruhusiwa kufanya mazoezi baada ya kujiunga na wachezaji wenzake wa Barcelona kwa mara ya kwanza leo.
    Nyota huyo wa Uruguay alilazimika kufanya mazoezi peek yake akisubiri majibu ya rufaa yake Mahakama ya Usuluhishi (CAS) juu ya adhabu ya kutojihusisha na soka kwa miezi mine baada ya kumng'ata Giorgini Chiellini wa Italia katika Kombe la Dunia. 
    CAS imepunguzia adhabu mchezaji huyo wa zamani wa Liverpool na sasa hataruhusiwa kucheza mechi za mashindano tu, lakini za kirafiki za klabu na timu ya taifa atacheza.
    Mkali huyo wa mabao mwenye umri wa miaka 27 atamaliza adhabu yake Oktoba na kuanza rasmi kucheza La Liga na Barca.

    Furaha: Luis Suarez amefanya mazoezi kwa mara ya kwanza na wachezaji wenzake wa Barca leo
    Content: Suarez was all smiles as he took part in his first Barcelona training session
    Suarez alikuwa mwenye furaha leo akifanya mazoezi na Barcelona kwa mara ya kwanza tangu asajiliwe
    A work out at last: Luis Suarez trains with his Barcelona team-mates on Friday, including club captain Xavi
    Luis Suarez akijifua na wachezaji wenzake wa Barcelona, akiwemo Nahodha Xavi
    All smiles: Barcelona are well under way with pre-season preparations, while Suarez has been training alone
    Barcelona wanaendelea na maandalizi ya msimu 
    Ready to go: Luis Suarez arrives for Barcelona training on Monday morning after a CAS ruling
    Luis Suarez akionyesha nembo ya Barcelona kwa furaha baada ya kupunguziwa adhabu na CAS 

    "Nina furaha sana kuwa tayari kujisikia kama mchezaji tena na kuwa na wachezaji wenzangu wa timu. Nilipagawa mno kuanza mazoezi,".
    "Nashukuru sana kwa tote ambayo klabu imenifanyia kwa wiki chache zilizopita. Wamenitendea wema mno na ninashukuru sasa kuwa tayari kuanza changamoto hii kubwa ya kuichezea Barca,".
    "Hayakuwa mazingira huru kabisa. Ni malipo ya makosa niliyoyafanya na ninaomba radhi, lakini natakiwa kuyaacha nyuma yangu yote sasa," amesema Suarez.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SUAREZ AANZA KUPIGA MZIGO LEO BARCA NA KUSEMA; "NAJISIKIA FURAHA KUWA MCHEZAJI TENA" Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top