• HABARI MPYA

    Tuesday, June 03, 2014

    ARSENAL DIZAINI WAMEDUNDA KWA BENZEMA, ASHIRIKI MATANGAZO YA JEZI MPYA REAL MADRID

    MABINGWA wa Ulaya, Real Madrid wamefichua jezi mpya za msimu ujao na katika kuashiria hawatamuachia Karim Benzema anayetakiwa na Arsenal, naye ametumia katika matangazo ya jezi hizo.
    Arsene Wenger amekuwa akimtaka kwa muda mrefu Mfaransa mwenzake huyo bila mafanikio na kwa sasa ni miongoni mwa wachezaji walio katika mipango yake baada ya kusaini Mkataba mpya wa miaka mitatu.
    Lakini katika tangazo la jezi mpya za vigogo hao wa Hispania, Gareth Bale na Karim Benzema wote wametumika.
    Msimu ujao wa 2014-2015, Cristiano Ronaldo na wenzake wataendelea kuvaa jezi zao za asili, nyeupe kwa mechi za nyumbani, ugenini watakuwa wanavaa pinki. Rangi ya tatu ni bluu.
    Watazame katika rangi ya pinki: Mabingwa wa Ulaya, Real Madrid wametambulisha jezi zao mpya za msimu ujao na Karim Benzema wa kwanza kulia anayetakiwa na Arsenal ameshiriki.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ARSENAL DIZAINI WAMEDUNDA KWA BENZEMA, ASHIRIKI MATANGAZO YA JEZI MPYA REAL MADRID Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top