• HABARI MPYA

    Wednesday, June 18, 2014

    UHOLANZI NOMAA, YATINGA 16 BORA MAPEMAAAA BAADA YA KUIFUMUA 3-2 AUSTRALIA

    UHOLANZI ni kama tayari imefuzu 16 Bora ya Kombe la Dunia kufuatia ushindi wa 3-2 dhidi ya Australia katika mchezo mgumu wa Kundi B Uwanja wa Beira-Rio mjini Porto Alegre nchini Brazil.
    Ushindi huo, unaifanya timu ya Louis van Gaal itimize ponti sita baada ya mechi mbili na kupaa kileleni mwa kundi hilo, ikiwa na mabao nane ya kufunga na matatu ya kufungwa.


    Rocket: Van Persie smashes a powerful strike into the roof of Australia's net to make it 2-2
    Roketi: Van Persie akiruka kushangilia baada ya kuifungia bao la kusawazisha Uholanzi dhidi ya Australia na 2-2 na chini anashangilia, wakati picha ya juu ni Robben akishangilia bao la kwanza aliloifungia Orange
    Jumping for joy: Manchester United striker Van Persie leaps into the air to celebrate his goal
    Mabao ya Uholanzi yamefungwa na Arjen Robben dakika ya 20, Robin Van Persie dakika ya 58 na Memphis Depay dakika ya 68, wakati mabao ya Australia yamefungwa na Tim Cahill dakika ya 21 na Mike Jedinak dakika ya 54 kwa penalti.
    Kikosi cha Australia kilikuwa: Ryan, McGowan, Wilkinson, Spiranovic, Davidson, Leckie, Jedinak, McKay, Oar/Taggart dk77, Bresciano/Bozanic dk51 na Cahill/Halloran dk69.
    Uholanzi: Cillessen, Martins Indi/Depay 45, Vlaar, De Vrij, Janmaat, De Jong, Blind, De Guzman/Wijnaldum dk78, Sneijder, Van Persie/Lens dk87 na Robben.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: UHOLANZI NOMAA, YATINGA 16 BORA MAPEMAAAA BAADA YA KUIFUMUA 3-2 AUSTRALIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top