Drogba |
KOCHA Roberto Di Matteo amesema Didier Drogba ana uwezo wa kubaki Chelsea
baada ya msimu huu.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34, mkataba wake
unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu na baada ya hapo imeelezwa atakubali
ofa ya kujiunga na Shanghai Shenhua ya China January.Di Matteo alisema anatarajiwa klabu hiyo itamhitaji tena mshambuliaji huyo.
“Kiwango cha Didier uimara wake vinamfanya astahili kuendelea kucheza Ligi Kuu akiwa Chelsea, au nyingine yoyote mwakani,” alisema Di Matteo kuwaambia Waandishi katika taarifa iliyotufikia bongopstaz.blogspot.com.
"Anaweza kuendelaea kucheza kwa miaka kadhaa katika kiwango hiki. Hatastaafu."
Di Matteo bado hana uhakika kama mwanasoka huyo wa kimataifa wa Ivory Coast atabakia Stamford Bridge katika kipindi chake kilichobaki kwenye soka, lakini anahisi mchezaji huyo tayari ni sehemu ya historia ya klabu hiyo.
"Iwe niwe popota, sijui," Di Matteo alisema. "Ni sehemu ya historia ya klabu, kama wachezaji wengi, na wakati wote itakuwa hivyo. Lakini uamuzi wa klabu,"alisema.
0 comments:
Post a Comment