• HABARI MPYA

    Saturday, April 21, 2012

    ARSENAL NA CHELSEA KAZI IPO LEO

    BAHATI mbaya iliyoje Chelsea inawasili Emirates ikiwa na lundo la majeruhi, kuliko wenyeji wao.
    The Gunners wamempoteza Mikel Arteta kwa mechi zote zilizobaki za msimu kwa maumivu ya kifundo cha mguu na anaungana na majeruhi wa muda mrefu Per Mertesacker, Jack Wilshere vifundo vya mguu kama yeye na Emmanuel Frimpong goti.
    Kuna habari njema kuhusu Francis Coquelin na Abou Diaby ambao wote wanatarajiwa kucheza mechi hiyo ya wapinzani wa Jiji la London, lakini Yossi Benayoun hataruhusiwa kucheza kwa mujibu wa mkataba wake mkopo kutoka The Blues.
    Chelsea itamkosa Branislav Ivanovic ambaye atakuwa anamalizia adhabu yake ya kusimamishwa mechi tatu baada ya mechi hii.
    Katika majeruhi, David Luiz anatarajiwa kukosa wiki nyingine kutokana na maumivu ya nyama za paja aliyoyapata kwenye Nusu Fainali ya Kombe la FA wakiifunga Tottenham.
    Ryan Bertrand ni majeruhi wakati Oriel Romeu anaumwa na wote hawatakuwapo leo.

    JE WAJUA?
    •Arsenal imeshinda mechi 12, sare mbili na kufungwa mechi mbili katika mechi zao 16 zilizopita Emirates.

    •The Gunners watamkosa Mikel Arteta kwa sehemu iliyobaki ya msimu na hawajashinda mechi ya Ligi Kuu bila ya yeye msimu huu.

    •Robin van Persie amefunga mabao 17 katika mechi 19 za klabu hiyo msimu huu.

     •Mshambuliaji huyo wa Kiholanzi, alipiga hat trick katika ushindi wa 5-3 kwenye mchezo wa kwanza Uwanja wa Stamford Bridge, ambako Arsenal iliweka rekodi ya kuwa timu ya kwanza tangu Liverpool mwaka 1996 kutikisa nyavu za Chelsea mara tano.

    •Chelsea imeshinda mechi tatu tu kati ya 19 zilizopita ikiwa mgeni wa Arsenal, lakini zote zinakuwa ni ndani ya mechi sita za mwishoni mwa msimu.

    •The Blues wamefungwa mabao mengi zaidi (18) katika dakika 15 za mwisho zaidi ya klabu nyingine yoyote kwenye Ligi Kuu.

    •Didier Drogba amefunga mabao manane katika Ligi Kuu dhidi ya The Gunners.

    •Chelsea imefunga na kufungwa asilimia 95 ya mabao yao ndani ya boksi – ambayo ni kiwango kikubwa katika ligi.

    VIKOSI VYA LEO:
    ARSENAL: Szczesny, Sagna, Koscielny, Vermaelen, Santos, Ramsey, Song, Rosicky, Walcott, Van Persie na Gervinho.

    CHELSEA: Cech, Bosingwa, Cahill, Terry, Cole, Lampard, Essien, Ramires, Mata, Sturridge na Torres.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ARSENAL NA CHELSEA KAZI IPO LEO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top