• HABARI MPYA

    Sunday, April 29, 2012

    HII NIMEIOKOTA FULL SHANGWE

    WATANZANIA WATAKIWA KUSHIRIKI PROMOSHENI YA "VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO" YA BIA ZA SERENGETI



    Na Mwandishi wetu
    KAMPUNI ya Bia ya Serengeti (SBL) imewataka watanzania kushiriki kwa nguvu  zote katika promosheni ya Vumbua Hazina ya Chini ya kizibo ili kuweza kushinda zawadi mbali mbali.
    Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Masoko wa Kambpuni ya SBL, Ephrahim Mafuru  na kusema kuwa SBL imetenga sh. Milioni 783 ambazo zitatolewa kama zawadi kwa washindi wa promosheni hiyo ambayo itafanyika kwa wiki 16 kuanzia Aprili 22.
    Mafuru alisema kuwa zawadi kwa wale watakao jishindia zawadi ya bia zina thamani y ash. Milioni 265 zawadi za fedha taslim ni sh. Milioni 383. Alisema kuwa pia watatoa pikipiki 16, Bajaj inane (8) , Jenereta nane (8) na magari matatu aina ya Ford Figo.
     Alisema kuwa ili kuweza kuingia katika shindano hilo unatakiwa kununua bia zao, Serengeti, Tusker au Pilsner  na kukuta neno  lenye tarakimu saba na kulituma kwenda namba maalum ya 15317 na kuingia katika shindano hilo.
    Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Push Mobile, Freddie Manento aliipongeza SBL kwa kuiteua kampuni yake kuendesha shindano hilo hasa kwa kuzingatia ubora wa huduma zake.
    Manento alisema kuwa kampuni yao ni bora zaidi katika kuendesha zoezi kama hilo na kuahidi kutoa hudima bora kwa wateja wake.
    “Ni faraja kubwa kufanya kazi na SBL katika shindano hili kubwa la kuwazawadia wateja wa bidhaa zinazozalishwa na kampuni hiyo ya bia, tutafikisha lengo lililowekwa,” alisema Manento.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: HII NIMEIOKOTA FULL SHANGWE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top