• HABARI MPYA

    Monday, April 30, 2012

    KAJALA AANGUA KILIO KIZIMBANI


    KAJALA AMWAGA CHOZI KORTINI



     Happiness Katabazi
    MSANII wa Filamu nchini, Kalaja Masanja leo alimwaga machozi na kuuujia juu upande wa Jamhuri katika kesi inayomkabili ya utakajitishaji fedha haramu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, akiushinikiza ulete mashahidi haraka kwani kule gerezani anakoishi siyo sehemu ya starehe.
    Kajala alitoa shinikizo hilo jana mbele ya Hakimu Mkazi Sundi Fimbo muda mfupi baada ya  Taasisi ya Kuzuia na Kupamba na Rsuhwa (PCCB), Swai kuikumbukusha mahakama kuwa kesi hiyo ilikuja jana kwaajili ya mashahidi wa upande wa Jamhuri kuanza kutoa ushahidi wao lakini akadai hilo halitaweza kufanyika kwasababu hajaja na mashahidi  na kwamba anaiomba kesi hiyo iarishwe.
    Baada ya wakili huyo wa PCCB kumaliza kutoa maelezo hayo ndipo Kajala akanyosha kidole na kuomba ruhusa ya mahakama ili aweze kuzungumza jambo na alizungumza kama ifuatavyo:
    “Mweshimiwa hakimu hivi huyu wakili wa serikali anafikiri kule gereza la Segerea ninakoishi kwa sasa ni  sehemu ya stahere? Gerezani kunatisha  wewe wakili wa serikali lete mashahidi  kesi isikilizwe”alidai Kajala huku akitokwa na machozi.
    Kwa upande wake Hakimu Fimbo aliarisha kesi hiyo Mei 9 mwaka huu,ambapo upande wa jamhuri unatakiwa ulete mashahidi wake ili waanze kutoa ushihidi.
    Machi 27 mwaka huu, ilidaiwa na wakili Swai kuwa Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU) Leonard Swai  alidai mbali na Kajala mshtakiwa mwingine ni muwe  Faraja Chambo  wanakabiliwa na makosa matatu, kosa la kwanza ni la kula njama kinyume na kifungu cha 34 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya mwaka 2007 ambapo washtakiwa wote kwa pamoja walitenda kosa hilo la kula njama la kuamisha umiliki wa nyumba iliyopo Kunduchi Salasala eneo ambalo halijapimwa jijini Dar es Salaam. 

    Shtaka la pili ni ni kwamba Aprili 14 mwaka 2010 waliamisha isivyo halali umiliki wa nyumba hiyo ambayo walikuwa wakiimiliki kwenda kwa Emilian Rugalia ambaye ndiyo walimuuzia kinyume na kifungu cha 34(2)A(3) cha Sheria ya TAKUKURU ya mwaka 2007. Na shtaka la tatu ni la kutakatisha fedha ambalo walilitenda siku hiyo ya Aprili 14 mwaka 2010 huku wakijiua ni kinyume na sheria hiyo. 

    Chambo ambaye naye yupo  gerezani  kwa zaidi ya mwaka mmoja kwasababu anakabiliwa na kesi nyingine ya utakatishaji fedha haramu iliyofunguliwa mahakamani hapo ambapo kwa mujibu wa sheria kosa hilo halina dhamana.

    SOURCE: DINA ISMAIL (mamapipiro.blogspot.com)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KAJALA AANGUA KILIO KIZIMBANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top