• HABARI MPYA

    Monday, April 30, 2012

    TUNAHITAJI UKUMBI BORA WA NDONDI


    Mchezo wa ngumi katika nchi yetu ya Tanzania unazidi kushika kasi
    kutokana na kuchipuka kwa mabondia wengina mapromota ambao wanapigana
    katika kuwania mataji mbalimbali nje na ndani ya Tanzania na kuandaa
    mapambano . wapo mabondia wengi katika historia ya Tanzania ambao
    wamewahi kupigana nje ya nchi hukiwauliza kuhusu ubora wa mchezo wa
    ngumi katika upande wa vifaa vya mchezo huo ndani ya nchi yetu ni
    imani yangu waliowengi wanaweza kukubaliana nami kuwa bado unahitaji
    vitu muhimu ili kuendeleza mchezo huo .
    
    Kwa Tanzania tumekuwa na mabondia wengi ambao wameweza kutingisha nje
    ya Tanzania kama Joseph Marwa, Rashid Matumla, Rogers mtagwa Ally Kimweri na
    Emanuel Mrundwa ambao waliweza kutwaa mataji mbalimbali ya mchezo huo
    . jambo moja kuu ambalo watanzania tunalisahau ni kukosekana kwa kumbi
    bora ya mchezo huo kwa upande mwingine kuna wakati baadhi ya watu
    wanaohusika na mchezo wa ngumi waliwahi kuwa na wazo hilo lakini
    nimeona jumatatu ya leo nijaribu kulitilia mkazo .natoa mfano kama
    tulivyo weza kujenga uwanja wa taifa na kuziona nchi kubwa duniani
    zikija kucheza mechi za kirafiki kama Brazil basi hata mchezo wa ngumi
    linawezekana ukitazama kama marekani ambao mchezo huu umekuwa kwa
    kiwango cha juu kutokana nchi hiyo kuboresha maeneo ya kuchezea
    kumbuka silinganishi kiwango cha mchezo bali ni namna ya kuboresha.
    
    Kwa Tanzania vipo vyama vingi vya mchezo wa ngumi PST,TPBC,TPBO bila
    kusahau kile cha taifa cha BFT lakini ni mara kadhaa Makore Mashaga
    katibu mkuu wa BFT amekuwa akizungumzia juu ya ukosefu wa vifaa maeneo
    ya mazoezi na kumbi za kupigania vimekuwa ni vikwazo vikubwa kwa
    mchezo huo kwa Tanzania kwakuwa serikali imeweza kuleta uwanja mpya wa
    mpira wa miguu ambao hata Suleiman nyambui anafaidika nao alikadharika
    wanamuziki kupata studio ya kisasa ya kurekodia muziki bila shaka
    mchezo wa ngumi nao unahitaji eneo zuri la kuchezea mchezo huo kama
    ilivyo Las Vegas Nevada na MGM Grand au Madson square ni dhahiri
    inawezakana kwa Tanzania kuwa na kumbi bora ya kisasa na imani vyama
    vya mchezo wa ngumi vyote nchini vinaweza kukaa chini na kujadiliana
    na serikali kupitia wizara ya habari utamaduni na michezo kuhakikisha
    tunapata kumbi bora ya kisasa ya kupigania ili kuongezea ujuzi na
    viwango vya mchezo wa ngumi kwa Tanzania.
    
    kama ufilipino imeweza kutoa bingwa wa dunia hata Tanzania inaweza pia
    kwani ukiacha soka mchezo wa ngumi ndio mchezo pekee ambao unakuja kwa
    kasi pengine liwe ombi rasmi kwa Rais wa jamhuri ya muungano wa
    Tanzania ambaye mwaka jana alitunikiwa tuzo ya heshima ya mwanamichezo
    na chama cha waandishi wa habari za michezo Tanzania TASWA kuwa
    kiongozi bora kwa kujari michezo si vibaya Mh Jakaya Kikwete
    akatuachia wapenzi wa masumbwi kumbi bora w hata mabondia wanje
    wajekupambana Tanzania kama zinavyokuja timu kubwa za mpira dunia
    kucheza uwanja wa taifa .
    
    nina maliza kwa kusema kuwa ni imani yangu kuwa kwa kujengwa uwanja
    huo kutawapa mabondia wa tanzania kujiaamini na kuupanua mchezo huo
    na unaweza pia kulitangaza jina la Tanzania katika Nyanja za utalii
    ndani na nje ya Tanzania kama inavyowezekana kuleta mastaa wa wakubwa
    wa muziki kutoka ulaya na amerika ni dhahiri hakuna lisilowekana kwa
    Tanzania .
    
    -- 
    Super D Boxing Coach
    Email.superdboxingcoach@gmail.com
    www.burudan.blogspot.com
    www.superdboxingcoach.blogspot.com
    Mob;+255787 406938
    +255774406938
    Po.Box. 15493
    Dar es Salaam Tanzania
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TUNAHITAJI UKUMBI BORA WA NDONDI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top