• HABARI MPYA

    Sunday, May 28, 2017

    SAMATTA AFIKISHA MABAO 20 GENK IKIUA 3-0 UBELGIJI

    Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
    MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta usiku wa jana amefunga bao la tatu timu yake, KRC Genk ikishinda 3-0 ugenini dhidi ya Sint-Truiden Uwanja wa Luminus Arena mjini Genk, Ubelgiji kwenye mchezo wa Kundi B kuwania tiketi ya kucheza michuano ya UEFA Europa League mwakani.
    Hilo linakuwa bao lake la 20 Samatta katika mechi 59 tangu ajiunge na Genk Januari mwaka jana akitokea TP Mazembe ya DRC. Na kwa ushindi huo, Genk inaendelea kuongoza Kundi B katika kuwania tiketi ya Europa League 2018 ikifikisha pointi 26 baada ya kucheza mechi 10.
    Samatta alifunga lake dakika ya 55 jana akimalizia pasi ya beki wa Jamhuri ya Czech, Jakub Brabec, baada ya kiungo mkongwe Mbelgiji mwenye umri wa miaka 36 Thomas Buffel kufunga la kwanza dakika ya 32 na kiungo Mholanzi, Jean-Paul Boetius kufunga la pili dakika ya 43.
    Mbwana Samatta (kulia) akishangilia baada ya kufunga bao lake la 20 jana Genk

    Kati ya mechi hizo 59, michezo 18 Samatta alicheza msimu uliopita na 41 msimu huu na kati ya hiyo, ni michezo 37 tu ndiyo alianza, 10 msimu uliopita na 27 msimu huu.
    Mechi 21 kati ya hizo alitokea benchi, nane msimu uliopita na 13 msimu huu, wakati 11 hakumaliza baada ya kutolewa, tano msimu uliopita na sita msimu huu na katika mabao hayo 19, 14 amefunga msimu huu na tano msimu uliopita.
    Kikosi cha KRC Genk jana kilikuwa: Ryan, Uronen, Colley/Janssens dk84, Brabec, Castagne, Berge, Malinovskyi/Heynen dk70, Writers, Boetius/Naranjo dk76, Buffalo na Samatta.
    STVV: Pirard, Mechele, The Petter, Peeters/Sart dk62, Gerkens, Ceballos/Abrahams dk77, Dussaut/Bagayoko dk71, Kotysch, Fernandes, Vetokele na Bolingoli.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SAMATTA AFIKISHA MABAO 20 GENK IKIUA 3-0 UBELGIJI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top