Monday, November 03, 2014

    VAN GAAL AMUITA SMALLING 'PUMBAVU' KWA KUTOLEWA NA NYEKUNDU JANA DHIDI YA MAN CITY

    KOCHA Louis van Gaal amemuita Chris Smalling ‘pumbavu’ kwa kujiruhusu kutolewa nje katika katika mechi dhidi ya mahasimu wa Jiji la Manchester, Man City ambayo United ilipoteza na kujikuta katika mwanzo mbaya zaidi ndani ya misimu 28.
    Sergio Aguero aliifungia bao pekee City dakika ya 63 kwenye ushindi huo wa 1-0 lakini kosa hilo lilitangulia dakika sita kabla wakati Smalling alipomkwatua James Milner na kupewa kadi ya pili ya njano na refa Michael Oliver, baada ya awali kupewa pia njano kwa kumchezea rafu kipa Joe Hart.
    "Katika mechi ya mahasimu unatakiwa kuwa makini — kadi ya pili ya njano ni kadi ya njano ya kipumbavu,’ amesema Van Gaal. "Ya kwanza sikuona, lakini kama mchezaji ukiwa na ya njano, unatakiwa kuifanyia kazi. Unatakiwa kujidhibiti katika mchezo wake. Nawaambia hivi wachezaji,"

    Chris Smalling akimpitia James Milner kabla ya kulimwa kadi ya pili ya njano
    United could have few complaints about the sending off, after Smalling showed naivety at the Etihad
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: VAN GAAL AMUITA SMALLING 'PUMBAVU' KWA KUTOLEWA NA NYEKUNDU JANA DHIDI YA MAN CITY Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry