• HABARI MPYA

    Thursday, November 13, 2014

    SUNDERLAND YATIWA HATIANI BAADA YA 'KUMZINGUA' REFA JUMAPILI WAKITOA DROO NA EVERTON

    KLABU ya Sunderland imetiwa hatiani na Chama Soka England kwa kushindwa kuwadhibiti wachezaji wake Jumapili wakitoka sare ya 1-1 na Everton Uwanja wa Light.
    Wachezaji wa Sunderland waliudhiwa na maamuzi ya refa, Lee Mason kuwapa penalti Toffees dakika ya 76 baada ya Connor Wickham kuangushwa na Seamus Coleman kwenye boksi.
    Leighton Baines hakufanya makosa baada ya kwenda kuukwamisha nyavuni mkwaju kufuatia Sebastian Larsson kuwapatia Black Cats bao la kuongoza dakika ya tisa kwa shuti la mpira wa adhabu.
    Coleman is felled by the challenge that led to a long period of deliberation by the officials 
    Seamus Coleman akienda chini baada ya kukutana na Connor Wickham kwenye mchezo huo jumapili
    Referee Lee Mason consults with his assistant after the incident inside the penalty area 
    Refa Lee Mason akiwasiliana na Msaidizi wake, baada ya tuklio hilo ndani ya eneo la penalti 
    Wickham remonstrates with the assistant but was lucky to not be sent off for the tackle
    Wickham na wachezaji wengine wa Sunderland walizozana na refa msaidizi baada ya Everton kupewa penalti

    Taarifa ya FA imesema: "Sunderland imetiwa hatiani na FA kufuatia mchezo wao na Everton Novemba 9, 2014. Imeelezwa kwamba katika dakika ya 76 ya mchezo, klabu ilishindwa kuwadhibiti wachezaji wake na klabu imepewa hadi saa 12 jioni ya Novemba 17, 2014 kujibu mashitaka hayo,".
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SUNDERLAND YATIWA HATIANI BAADA YA 'KUMZINGUA' REFA JUMAPILI WAKITOA DROO NA EVERTON Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top