• HABARI MPYA

    Wednesday, November 05, 2014

    DAVID JAMES SASA AUZA ZAGAZAGA ZAKE HADI ZA NDANI BAADA YA KUFILISIKA

    KIPA wa zamani wa England, David James amelazimika kuweka mnadani jezi, bukta na mipira aliyoisaini baada ya kuwekwa wazi Mei mwaka huu kwamba amefilisika.

    KIPA WA ZAMANI WA ENGLAND ALIVYOFULIA LICHA YA KUINGIZA PAUNI MILIONI 20

    GONGA HAPA kusoma zaidi David James alivyofilisika
    James, ambaye hivi karibuni amekatisha ustaafu wake na kuwa kocha mchezaji wa timu ya Ligi Kuu ya India, Kerala Blasters FC, amejikuta mufilisi baada ya kuachana na mkewe mwaka 2005.
    Mlinda mlango huyo mwenye umri wa miaka 44, who amechezwa timu kadhaa Ligi Kuu England kama Liverpool, Manchester City na Portsmouth enzi zake na inaelezwa alivuna kiasi cha Pauni Milioni 20 wakati huo.

    Former Premier League goalkeeper James won the FA Cup with Portsmouth in 2008
    James akiinua Kombe la FA alilotwaa akiwa na Portsmouth mwaka 2008
    James made 53 appearances for England, including in the 2010 World Cup in South Africa
    James aliichezea mechi 53 England, ikiwemo za Kombe la Dunia mwaka 2010 nchini Afrika Kusini

    James ameamua kuuza zagazaga kadhaa kama 150 hive alizotia saini yake kupitia kampuni ya Kent-based auctioneer Hilco.

    "Watu watalazimika kupambana kwa dau kununua bidhaa hizo, ambazo ni pamoja na vifaa vya soka, muziki na sanamu, kuanzia Novemba 6 hadi 18,".

    Jezi ya Frank Lampard iliyosainiwa, nguo ya kudakia ya pinki ya Portsmouth na jezi ya NFL ni miongoni mwa bidhaa 150 zilizotiwa mnadanai na James.
    Kipa huyo pia ameweka mnadani jezi aliyopewa na kipa wa Chelsea, Petr Cech mwaka katika fainali ya Kombe la FA mwaka 2010 dhidi ya Portsmouth, jezi ya Uholanzi aliyobadilishana na Edwin van der Sar na jezi ya Michael Owen Namba 10 yenye salamu za 'kila la heri' zilizoandikwa. Hilco are also selling a V-reg purple three-door Vauxhall Astra as part of the auction for James
    Hilco pia wanauza V-reg ya rangi ya zambarau, Vauxhall Astra ya milango mitatu kama sehemu ya bidhaa za James zilizotiwa sokoni

    MIAKA 26 YA DAVID JAMES KATIKA SOKA...

    Umri: Miaka 44
    Klabu ya sasa: Kerala Blasters (Kocha/Mchezaji)
    Mechi alizoichezea England: 53 (Kuanzia 1997 hadi 2010)
    Mechi rasmi alizozichezea klabu: 947 
    Klanu za zamani: Watford, Liverpool, Aston Villa, West Ham, Manchester City, Portsmouth, Bristol City, Bournemouth, IBV (Iceland)
    Mataji: Kombe la Ligi (1995), Kombe la FA (2008) 
    James played 134 league games for Portsmouth between 2006-2010, winning the FA Cup in 2008
    James amecheza mechi 134 akiwa Portsmouth kati ya 2006 hadi 2010, akishinda nayo Kombe la FA mwaka 2008
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: DAVID JAMES SASA AUZA ZAGAZAGA ZAKE HADI ZA NDANI BAADA YA KUFILISIKA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top