• HABARI MPYA

    Wednesday, November 05, 2014

    MAN UNITED WAJIACHIA NA WAKE NA VIMADA WAO KATIKA USIKU AMBAO LIVERPOOL NA ARSENAL ZILITESEKA ULAYA

    KLABU ya Manchester United imechangisha kiasi cha Pauni 210,000 katika hafla ya hisani ya 15 ya ushirikiano wao na Shirika la Watoto la Umoja wa Mataifa (UNICEF) iliyoambataa na chakula cha usiku jana. 
    Katika usiku ambao hisia za Waingereza wengi zilikuwa Madrid na London kwenye mechi za Ligi ya Mabingwa Ulaya, Louis van Gaal na wachezaji wake walikutana Old Trafford kuchangisha fedha hizo kwa ajili ya shirika hilo la watoto. 
    Wachezaji wengi wa United walihudhuria sherehe hiyo na wapenzi wao na wake zao na wakapiga nao picha nje ya Uwanja.  
    Wakati shughuli hiyo, inaendelea Arsenal jana ililazimishwa sare ya 3-3 na Anderlecht Uwanja wa Emirates na Liverpool ikafungwa 1-0 na Real Madrid katika mechi za Ligi ya Mabingwa. 
    Wachezaji wa Manchester United wakionyesha wanajali baada ya kutoa kuhudhuria hafla ya chakula cha usiku ya klabu yao na UNICEF
    Angel Di Maria and wife Jorgelina were at the dinner
    Tyler Blackett and partner Naomi Thomas
    Angel Di Maria na mkewe Jorgelina walikuwepo kwenye sherehe hiyo, wakati kulia ni Tyler Blackett na mpenzi wake, Naomi Thomas 

    PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2821261/Manchester-United-players-wives-help-raise-210-00-charity-Gala-Dinner.html#ixzz3IBAVK4dr 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN UNITED WAJIACHIA NA WAKE NA VIMADA WAO KATIKA USIKU AMBAO LIVERPOOL NA ARSENAL ZILITESEKA ULAYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top