• HABARI MPYA

    Saturday, October 11, 2014

    MBIO ZA EURO 2016; KEANE APIGA HAT TRICK IRELAND IKIUA 7-0, MABINGWA WA DUNIA UJERUMANI WATANDIKWA 2-0

    MSHAMBULIAJI Robbie Keane amefunga mabao matatu peke yake Jamhuri Ireland ikishinda 7-0 dhidi ya Gibraltar katika mchezo wa Kundi D kufuzu Euro 2016. 
    Keane alifunga mabao yake katika dakika za sita, 14 na 18 kwa penalti, wakati James McClean alifunga mawili dakika za 46 na 53, huku kipa wa Gibraltar, Jordan Perez akijifunga dakika ya 52 na Wesley Hoolahan akahitimisha sherehe hiyo ya mabao dakika ya 56.
    Robbie Keane akishangilia baada ya kupiga hat-trick Jamhuri ya Ireland ikishinda 7-0 dhidi ya Gibraltar

    Katika mechi nyingine za kundi hilo, Poland imeifunga 2-0 Ujerumani mabao ya Arkadiusz Milik dakika ya 51 na Sebastian Mila dakika ya 88 huku bao la kujifunga la Akaki Khubutia likiipa ushindi wa 1-0 Scotland dhidi ya Georgia.
    Mechi za kundi F, Romania imetoka 1-1 na Hungary sawa na Finland na Ugiriki, wakati Ireland Kaskazini imeichapa Faroe Islands 2-0 na Kundi I, Armenia imetoka 1-1 na Serbia sawa na Albania na Denmark. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MBIO ZA EURO 2016; KEANE APIGA HAT TRICK IRELAND IKIUA 7-0, MABINGWA WA DUNIA UJERUMANI WATANDIKWA 2-0 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top