Simba SC |
SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limeteua waamuzi kutoka
Swaziland kuchezesha mechi ya kwanza ya 16 bora ya Kombe la Shirikisho kati ya
Simba na Al Ahly Shandy ya Sudan itakayochezwa Aprili 29 mwaka huu Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam.
Waamuzi hao wa mechi hiyo namba 71 ni Nhleko Simanga
Pritchard atakayepuliza filimbi wakati wasaidizi wake ni Mbingo Petros
Mzikayifani na Sibandze Thulani. Mwamuzi wa mezani atakuwa Fakudze Mbongiseni
Elliot.
CAF pia imemteua Kayijuga Gaspard wa Rwanda kuwa Kamishna wa
mechi hiyo.
Wakati huo huo: Kampuni nne kati ya sita zimepita hatua ya
kwanza ya mchakato wa kupata moja itakayofanya kazi ya kutengeneza tiketi za
elektroniki kwa ajili ya mechi za Ligi Kuu ya Vodacom na nyingine
zinazosimamiwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
Shughuli ya ufunguzi wa maombi ya hatua ya awali ya kuonesha
nia (Expression of Interest) kwa ajili ya tenda hiyo ilifanywa jana (Aprili 19
mwaka huu) na Kamati ya Mipango na Fedha ya TFF ambayo ndiyo Bodi ya Tenda ya
shirikisho.
Kampuni ambazo zimepita hatua hiyo ya kwanza sasa zinatakiwa
kuwasilisha rasmi tenda zao kwa ajili ya shughuli hiyo ndani ya kipindi cha wiki
tatu tangu ulipofanyika ufunguzi wa hatua ya kwanza.
Baadaye Bodi ya Tenda itakutana tena kupitia tenda
zitakazokuwa zimewasilishwa na kufanya uteuzi wa kampuni moja itakayofanya kazi
hiyo.
Kampuni ambazo zimefanikiwa kuingia katika hatua hiyo ya pili
ni CRDB Bank PLC, SKIDATA People Access Inc., Prime Time Promotions na
Punchlines (T) Limited.
0 comments:
Post a Comment