• HABARI MPYA

    Tuesday, April 17, 2012

    NDUGU YAKE OKWI KUCHEZESHA NGORONGORO NA SUDAN

    Thomas Ulimwengu, tegemeo la Ngorongoro
    SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limewateua waamuzi kutoka Uganda, nchi anayotoka mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi kuchezesha mechi ya michuano ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 kati ya Tanzania (Ngorongoro Heroes) na Sudan itakayofanyika Aprili 21 mwaka huu.
    Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniphace Wambura ameiambia bongostaz.blogspot.com mchana huu kwamba refa atakayechezesha mechi hiyo itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni ni Brian Miiro.
    Wambura amesema Waamuzi wasaidizi ni Mark Ssonko na Lee Patabali wakati mwamuzi wa mezani ni Denis Batte.
    Ejigu Ashenafi wa Ethiopia ndiye ameteuliwa kuwa Kamisaa wa mechi hiyo namba 15.
    Kamisaa na waamuzi hao watawasili nchini Aprili 19 mwaka huu kwa ndege za Ethiopian Airlines na Air Uganda.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NDUGU YAKE OKWI KUCHEZESHA NGORONGORO NA SUDAN Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top