TIMU ya Hispania imetoa suluhu (0-0) na Cape Verde katika mchezo wa Kundi H Fainali za Kombe la Dunia usiku huu Uwanja wa Mercedes-Benz Jijini Atlanta, Georgia nchini Marekani.
Sifa zimuendee kipa mkongwe wa umri wa miaka 40, Josimar José Évora Dias ‘Vozinha’ wa klabu ya Chaves ya Ureno aliyedaka kwa ustadi mkubwa na kuokoa michomo mingi ya hatari kuisaidia Cape Verde kupata suluhu hiyo ikicheza Fainali za Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza kihistoria.
Mchezo mwingine wa Kundi H utafuatia baadaye kati ya Saudi Arabia na Uruguay kuanzia Saa 7:00 usiku Uwanja wa Hard Rock, Miami Gardens, Florida, Marekani.
Mchezo mwingine wa Kundi H utafuatia baadaye kati ya Saudi Arabia na Uruguay kuanzia Saa 7:00 usiku Uwanja wa Hard Rock, Miami Gardens, Florida, Marekani.



.png)
0 comments:
Post a Comment