YANGA NA RUVU SHOOTING KATIKA PICHA JANA 'SHAMBA LA BIBI'
Winga wa Yanga, Simon Msuva akiupigia hesabu mpira mbele ya wachezaji wa Ruvu Shooting katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jana Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Yanga ilishinda 2-1
Beki wa Ruvu Shooting, Shaibu Nayopa (kulia) akiokoa mpira mbele ya mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma (kushoto)
Nayopa (kulia) akitafuta maarifa ya kumpokonya mpira mshambuliaji wa Yanga, Amissi Tambwe (kushoto)
Kiungo Haruna Niyonzima wa Yanga (kushoto) akimpita kiungo wa Ruvu, Issa Kanduru
Beki wa Yanga, Andrew Vincent akiwania mpira wa juu dhidi ya mshambuliaji wa Ruvu, Fully Zulu Maganga
Mshambuliaji wa Yanga, Obrey Chiwa (kushoto) akimpira beki wa Ruvu, Renatus Kisase
Beki wa Ruvu, Mau Ally Bofu (kulia) akimiliki mpira pembeni ya beii wa Yanga, Hassan Kessy
Wafungaji wa mabao ya Yanga jana, Simon Msuva (kushoto) na Haruna Niyonzima (kulia) wakishangilia mbele ya wapicha piga wa vyombo mbalimbali vya Habari
Kikosi cha Yanga kabla ya mchezo wa jana Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam
Kikosi cha Ruvu Shooting kabla ya kuanza kwa mchezo wa jana Uhuru
0 comments:
Post a Comment