• HABARI MPYA

    Thursday, May 07, 2015

    TIMU TANO ZAWANIA NAFASI MOJA TU YA KUBAKI LIGI KUU, NDANDA, MGAMBO ZATEGEMEA HURUMA ZA YANGA, AZAM

    Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
    PAZIA la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara litafungwa Jumamosi ya Mei 9, mwaka huu kwa mechi saba kuchezwa viwanja tofauti.
    Polisi Moro imekwishaipa mkono wa kwaheri Ligi Kuu na kundeleza rekodi yake ya kupanda na kuteremka msimu huo huo, wakati Ruvu Shooting, Prisons, Ndanda FC, Mgambo Shooting na Stand United zitakuwa zinagombea nafasi moja ya kubaki Ligi Kuu.


    Ndanda wanacheza na Yanga SC ambayo tayari imeweka kabatini Kombe la ubingwa wa Ligi Kuu, je watapata huruma ya Jangwani wasiteremke daraja?

    RATIBA MECHI ZA MWISHO LIGI KUU

    Mei 9, 2015
    JKT Ruvu Vs Simba SC
    Mtibwa Vs Coastal Union 
    Stand Utd Vs Ruvu Shoot
    Mbeya City Vs Polisi Moro
    Kagera Sugar Vs Prisons
    Ndanda FC Vs Yanga SC
    Azam FC Vs Mgambo JKT 

    Ndanda wenye pointi 28 wanacheza na Yanga SC, ambayo tayari imetwaa ubingwa, Mgambo Shooting yenye pointi 28 wanacheza na Azam FC ambayo tayari imejinyakulia nafasi ya pili.
    Timu hizo mbili kama zitapata ‘huruma’ ya wapinzani wao, Yanga na Azam na kushinda, maana yake zitafikisha pointi 31 na kuepuka balaa la kushuka.
    Stand United yenye pointi 28 itakuwa mwenyeji wa Ruvu Shooting yenye pointi 29, zote zina hali mbaya, wakati Polisi Moro yenye pointi 25 itakuwa mgeni wa Mbeya City yenye pointi 31, na Prisons wenye pointi 28 watakuwa wageni wa Kagera Sugar yenye pointi 31.

    MSIMAMO WA LIGI KUU YA VODACOM TZ BARA 

    1     Yanga SC    25   17   4     4     52   17   35   55  
    2     Azam FC      25   13   9     3     36   18   18   48  
    3     Simba SC    25   12   8     5     36   18   18   44  
    4     Mtibwa        25   7     10   8     24   24   0     31  
    5     Mbeya City  25   7     10   8     21   22   -1    31  
    6     Kagera         25   8     7     10   22   26   -4    31  
    7     JKT Ruvu     25   8     7     10   19   23   -4    31  
    8     Coastal U     25   7     10   8     19   24   -5    31  
    9     Ruvu Shoot  25   7     8     10   16   28   -12 29  
    10   Prisons         25   5     13   7     18   22   -4    28  
    11   Ndanda        25   7     7     11   20   29   -9    28  
    12   Mgambo     25   8     4     13   18   28   -10 28  
    13   Stand Utd   25   7     7     11   22   34   -12 28
    14   Polisi Moro 25   5     10   10   16   26   -10 25

    Timu za Ligi Kuu msimu ujao zitaongezeka kutoka 14 hadi 16 na msimu huu timu zitashuka timu mbili, huku tayari timu za kupanda ni Majimaji ya Songea, Mwadui ya Shinyanga, Toto Africans ya Mwanza na African Sports ya Tanga. 
    Timu ipi itaungana na Polisi Moro kuipa mkono wa kwaheri Ligi Kuu? Bila shaka hilo ni jambo la kusubiri na kuona.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TIMU TANO ZAWANIA NAFASI MOJA TU YA KUBAKI LIGI KUU, NDANDA, MGAMBO ZATEGEMEA HURUMA ZA YANGA, AZAM Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top