'WACHOVU' Bayern Munich wamefungwa bao 1-0 nyumbani na Augsburg katika mechi ya Bundesliga leo, hicho kikiwa kipigo cha nne mfululizo amacho kinakatisha tamaa kuelekea mchezo wa marudiano wa Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na Barcelona.
Bao pekee la Augsburg limefungwa na Raul Bobadilla dakika ya 71 huo ukiwa ushindi wao wa kwanza daima Uwanja wa Allianz Arena.
Kocha Pep Guardiola aliwapumzisha nyota wake kadhaa kwa ajili ya mechi na Barcelona Jumanne, kufuatia kufungwa mabao 3-0 katika mchezo wa kwanza Hispania.
Kipa wa zamani wa Liverpool, Pepe Reina akionyeshwa kadi nyekundu dakika ya 13 tu ya mchezo huo PICHA ZAIDI GONGA HAPA
The Bavarians sasa wanapoteza mechi ya nne mfululizo, baada ya vipigo vya awali kutoka kwa Borussia Dortmund katika Kombe la Ujerumani, Bayer Leverkusen katika Ligi na Barcelona katika Ligi ya Mabingwa wiki hii.
Kipa wa pili, Pepe Reina alimchezea rafu mshambuliaji wa Argentina, Bobadilla katika boksi akatolewa kwa kadi nyekundu na kulazimisha kipa wa kwanza, Manuel Neuer aingie. Guardiola sasa amekali 'kuti kavu' Munich kutokana na matokeo haya.


.png)
0 comments:
Post a Comment