// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); ZAMBIA SARE 1-1 NA DRC AFCON - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE ZAMBIA SARE 1-1 NA DRC AFCON - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Sunday, January 18, 2015

    ZAMBIA SARE 1-1 NA DRC AFCON

    ZAMBIA imelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 leo na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) katika mchezo wa Kundi B Fainali za Mataifa ya Afrika zilizoanza jana nchini Equagorial Guinea.
    Given Singuluma alitangulia kuifungia Chipolopolo dakika ya pili ya mchezo, kabla ya Yannick Bolasie kuisawazishia DRC dakika ya 66.
    Mechi nyingine ya Kundi hilo, kati ya Tunisia na Cerpe Verde itaanza Saa 4:00 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.  
    Mechi za ufunguzi jana, Gabon ilijiweka kileleni mwa Kundi A kufuatia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Burkina Faso.
    Mshambuliaji wa Borussia Dortmund, Pierre-Emerick Aubameyang, aliifungia Gabon bao la kwanza dakika ya 19, kabla ya Malick Evouna kufunga la pili dakika ya 72.
    Gabon sasa inaanza na pointi tatu kileleni mwa kundi, mbele ya wenyeji Equatorial Guinea wenye pointi moja sawa na Kongo baada ya sare ya 1-1 baina yao, wakati Burkina Fasso inashika mkia ikiwa haina pointi.
    Bao la dakika ya 87 la Bifouma Koulossa liliinusuru Kongo kulala mbele ya Equatorial Guinea, baada ya Nsue Lopez kutangulia kuwafungia wenyeji dakika ya 16.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ZAMBIA SARE 1-1 NA DRC AFCON Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top