// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); TUNISIA NAYO YASHIKWA, 1-1 NA CERPE VERDE AFCON - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE TUNISIA NAYO YASHIKWA, 1-1 NA CERPE VERDE AFCON - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Monday, January 19, 2015

    TUNISIA NAYO YASHIKWA, 1-1 NA CERPE VERDE AFCON

    TIMU ya taifa ya Tunisia, imetoka sare ya 1-1 na Cape Verde katika mchezo wa Kundi B, Fainali za Mataifa ya Afrika usiku huu Uwanja wa Ebebiyín, Equatorial Guinea.
    Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Eric Arnaud Otogo-Castane, Mohamed Ali Moncer alitangulia kuifungia Tunisia dakika ya 70, kabla ya 
    Heldon Augusto Almeida Ramos kusawazisha kwa penalti dakika ya 77.
    Matokeo hayo yanamaanisha timu zote za Kundi B zinalingana kwa kila kitu baada ya mechi za kwanza Jumapili.
    Mapema Zambia ililazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 pia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Given Singuluma akitangulia kuifungia Chipolopolo dakika ya pili ya mchezo, kabla ya Yannick Bolasie kuisawazishia DRC dakika ya 66.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TUNISIA NAYO YASHIKWA, 1-1 NA CERPE VERDE AFCON Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top