// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); ARSENAL WAWAKALISHA MABINGWA ENGLAND, MAN CITY WAPIGWA 2-0 ETIHAD - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE ARSENAL WAWAKALISHA MABINGWA ENGLAND, MAN CITY WAPIGWA 2-0 ETIHAD - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Sunday, January 18, 2015

    ARSENAL WAWAKALISHA MABINGWA ENGLAND, MAN CITY WAPIGWA 2-0 ETIHAD

    ARSENAL wamewakalisha mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya England, Manchester City kwa mabao 2-0 katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Etihad usiku huu.
    Ushindi huo, unaifanya The Gunners ifikishe pointi 39 baada ya mechi 22 na kupanda hadi nafasi ya tano mbele ya Tottenham, wakati City inayobaki na pointi zake 47 inaendelea kukamata nafasi ya pili.
    Santi Carzolla alifungua biashara kwa bao la penalti dakika ya 24, kufuatia Nahodha wa City, Vincent Kompany kumchezea rafu Nacho Monreal kwenye eneo la hatari.
    Olivier Giroud akakamilisha ushindi wa pointi tatu muhimu kwa kikosi cha Arsene Wenger kwa bao la pili dakika ya 66.
    Kikosi cha Manchester City kilikuwa; Hart, Zabaleta, Kompany, Demichelis, Clichy, Fernandinho/Lampard dk63, Fernando, Jesus Navas/Dzeko dk76, Silva, Milner/Jovetic dk46 na Aguero.
    Arsenal: Ospina, Bellerin, Mertesacker, Koscielny, Monreal, Coquelin, Oxlade-Chamberlain/Rosicky dk66, Ramsey/Flamini dk84, Cazorla, Sanchez/Gibbs dk84 na Giroud.
    Giroud slides in jubilant celebration and is joined by Arsenal team-mate Alexis Sanchez as they head towards a crucial three points
    Giroud akiteleza kushangilia na mchezaji mwenzake wa Arsenal, Alexis Sanchez baada ya kufunga

    PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2915617/Manchester-City-0-2-Arsenal-Santi-Cazorla-s-penalty-Olivier-Giroud-s-header-earn-Gunners-rare-victory-Etihad-Stadium.html#ixzz3PCLPnFyC 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ARSENAL WAWAKALISHA MABINGWA ENGLAND, MAN CITY WAPIGWA 2-0 ETIHAD Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top