// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); NAHODHA WA COASTAL UNION NA WENGINE 15 WAHAMIA GOR MAHIA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE NAHODHA WA COASTAL UNION NA WENGINE 15 WAHAMIA GOR MAHIA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Friday, January 09, 2015

    NAHODHA WA COASTAL UNION NA WENGINE 15 WAHAMIA GOR MAHIA

    Wachezaji wapya wa Gor Mahia, Jerry Santo wa kwanza kushoto waliosimama

    WACHEZAJI WAPYA WA GOR MAHIA 

    Jerry Santo – kiungo kutoka Coastal Union
    David Onyango Magoma – mshambulizi kutoka Mawego Talent Academy
    Ali Abondo "Teargas' – kiungo kutoka Tusker FC
    Ronald Otieno Omino – straika kutoka Muhoroni Youth
    Earnest Wendo – kiungo mkabaji kutoka Bidco United
    Farouk Ssentongo – kiungo mshambulizi kutoka Uganda
    James Ohawa – straika kutoka Bombo FC ya Uganda
    Augustine Walusimbi – beki kutoka Masaka Local Council FC
    Dirkir Glay – beki kutoka Thika United
    Zachary Toufiq – straika kutoka Ghana
    Khalid Aucho – kiungo kutoka Tusker FC
    Martin Werunga – beki kutoka FC Talanta,  
    Michael Olunga straika kutoka Thika United, 
    Innocent Wafula –kiungo kutoka Chemelil Sugar
    Boniface Oluoch – kipa kutoka Tusker FC
    Bernard Odhiambo – beki kutoka Nakuru AllStars 
    Na Vincent Malouda, NAIROBI
    ALIYEKUWA nahodha wa Coastal Union ya Tanzania bara na mkenya Jerry Santo ni miongoni mwa wachezaji kumi na sita waliozinduliwa na mabingwa wa Kenya, Gor Mahia.
    Gor imo mbioni kujiandaa kombe la klabu bingwa barani Afrika na sasa imewasajili wachezaji kumi na sita kujaza nafasi za wachezaji walioondoka miongoni mwao Dan Sserunkuma aliyehamia Simba SC, Geoffrey ‘Baba’ Kizito kwenda Vietnam na David ‘Calabar’ Owino aliyejiunga na ZESCO United ya Zambia.
    Sasa Gor Mahia ina jumla ya wachezaji 28 na wanayo nafasi mbili kufanya sajili nyingine. 
    Taarifa kutoka ndani ya klabu hiyo zasema kuwa wana mikakati ya kumnasa straika la mahasimu wao wa jadi AFC Leopards Jacob Keli na vile vile nahodha wa Muhoroni Youth Abbas Akinyemi.
    Misimu miwili iliyopita, Santo aling'ara na Coastal Union ya Tanga katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara, hiyo ni klabu ya pili kuchezea nchini humo baada ya awali kuwa Simba SC ya Dar es Salaam.
    Kabla ya kurejea Kenya, Santo alijaribu kurejea Simba SC, lakini hakufanikiwa kutokana na kugoma kufanya majaribio kama alivyotakiwa na kocha wa Wekundu hao wakati huo, Mcroatia Zdravko Logarusic. Santo pia alikwenda Oman kujaribu kujiunga na Fanja ya huko bila mafanikio na hatimaye sasa amerudi nyumbani kujipanga upya. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NAHODHA WA COASTAL UNION NA WENGINE 15 WAHAMIA GOR MAHIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top